Mwanzo | | Maswali ya Kisheria
Maswali ya Kisheria

Shiriki swali

Hukumu ya Mafuta yanayotumika kulainisha uso

Swali:

      Kutokana na hali ya baridi watu huwa wanatumia mafuta kwa ajili ya kulainisha ngozi zao, na hali hii huwa ni kwa wingi na endelevu, sasa vipi mtu akawa anataka kuchukua udhu huku akiwa anajua kabisa kwamba masaa machache kabla alitumia mafuta?, je achukue udhu hivyohivyo au ni lazima kwanza aondoe mafuta yote?.

Jawabu:

             Kwa Jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma na mwenye kurehemu.

Ikiwa ambayo yamebakia ni mafuta ambayo hayazuii kufika kwa maji katika viungo vya udhu basi hakuna tatizo, lakini kama itakuwa yaliyobakia ni ukungu mzito basi ni lazima autoe kwanza.

                   Ayatollah Sheikh Muhammad Yaaqobiy

 

Shiriki swali

Hukumu ya wazazi wenye kuzuia watoto kufunga

Swali:

      Ni ipi hukumu ya wazazi ambao wanazuia  kufunga watoto wao ambao wameshafikia umri kwa kulazimikiwa na sheria, kwa hoja ya kwamba bado ni wadogo na hawataweza kufunga. Na watoto wana majukumu gani katika hili?.

Jawabu:

             Kitendo hichi cha wazazi kwanza si sahihi na ni kinyume na uchamungu, kama ambavyo pia ni kuwazembesha watoto mambo ya dini. Bali inatakiwa wazazi wawe kinyume chake, wawatie moyo na kuwapa mafunzo watoto wao kabla hata ya kubalehe, ili iwe rahisi kwao watakapofikia balehe.

Ama watoto wao ni lazima wafunge, kwani hakuna kumtii kiumbe katika kumuasi Mwenyezi Mungu, na ikitokea wamelazimishwa kula basi itabidi walipe baadae. Ila kama itakuwa kinachopelekea kulazimishwa kula ni jambo la kweli na lenye madhara basi hakuna ulazima wa kufunga kiasi kwamba wakaingia katika matatizo.

                   Ayatollah Sheikh Muhammad Yaaqobiy

 

Shiriki swali

Uharamu wa kutakatisha mali

Swali:

    Assalamu Alaykum:

Mimi ini mwanafunzi wa ngazi ya Masters katika chuo kikuu cha Almustafa mjini Qom Iran, na nipo katika kuandika Risala yenye maudhui ya “..Utakatishaji mali, mtazamo wa fiqhi na kanuni”, nimetafuta sana katika fatwa lakini sijapata rai yeyote ya maulama wetu wa Kishia kuhusu hili, ikumbukwe ni muhimu sana kuwa na rai za maulama wetu kunako jambo hili pamoja na kutaja chimbuko la hukumu ya hili linalojulikana sasa kwa kutakatisha mali.

 

Jawabu:

       Kwa jina la Mwenyezi Mungu

Utakatishaji mali ni katika mambo yenye kuharibu uchumi wa miji na kuharibu tabia na mienendo ya watu na hata kupoteza imani zao. Pia ni sababu ya kuwepo kwa mazingira ya ufisadi na jinai. Na hapo awali jambo hili lilikuwa likifanywa na makundi ya kiuhalifu, lakini kwa sasa imekuwa ni jambo la wote hasa wakubwa wa kisiasa na viongozi mbalimbali.

Na ulimwengu wa sasa umefanikiwa kutambua hatari ya jambo hili na kuamua kuweka makongamano mbalimbali yenye kulenga kuweka mikakati ya kuweza kufichua na kupambana nalo, ikiwa ni pamoja na kuweka kanuni za kupambana na wenye kufanya jambo hili.

Lakini tunaona bado hata haya makongamano hayajaweza kusimamia jambo hili kwa kiwango kikubwa, kutokana na kutokuwa na umakini mkubwa katika utendaji, au urafiki baina ya wenye kusimamia, bali inawezekana hata hao pia ndio wakawa wenye kushiriki jambo hilo, na ndio maana bado tunaona jambo hili linazidi kushamili katika jamii na nchi kwa ujumla.

Sasa tukija katika hukumu ya kisheria ni kwamba kuna mambo matatu yenye kuamuaaina ya hukumu:       

1.   Chenye kutakatishwa, kwa maana ya zile mali ambazo  hutakatishwa, kuna wakati zinakuwa ni mali za haramu ambazo zimepatikana kwa njia ya wizi au biashara za madawa, rushwa nk. Na mara nyingi hapa hufanyika jambo la kuzitakatisha kwa kutafuta uhalali wake kwa kuziweka katika benki, sasa kama asili ya mali itakuwa ni haramu basi tendo hili lote linakuwa ni haramu.    

2.   Mtakatishaji, kwa maana ya mtu au upande unaotumika kutakatisha hizo mali. Kuna wakati zinakuwa zinakuwa ni njia ambazo haifai kufanya kazi kama vile vikundi vya kihalifu, kigaidi, viongozi wenye kukandamiza raia wao, madikteta nk. Hivyo inakuwa ni haramu kwa njia ya kuwapa hawa watu waweze  kusimamia jambo la kutakatisha fedha, kutokana na uharamu wa kudhamini au kuwatia nguvu hawa watu, na hapa ni bila ya kuangalia   kipengele cha kwanza cha kitendo.

3.   Utakatishaji wenyewe,    kwa maana ya zile sehemu zenyewe ambazo zinasimamia kitendo cha kutakatisha na kuzipeleka katika mabenki au mashirika ya kimali, hivyo inawezekana ikawa i haramu kwa upande wa kwamba huyu mwenye kusimamia  jambo hili akawa hana kibali cha sheria au ikawa huyo msimamizi ndio fisadi.

Hivyo kwa mujibu wa haya tunaweza sema kuwa uharamu unaweza kupatikana kwa moja ya sababu hizo tatu, na pia kwa kuongezea ni kwamba kuna sababu nyinginezo ambazo zinaweza kuwa chanzo cha uharamu, nazo ni:    

·       Wenye akii wote wamekubali kwamba jambo hili linapelekea kuhujumu uchumi, hivyo hili ni jambo ambalo tunasema ni lenye kuhujumu na kuharibu maisha ya watu na si mtu mmoja kama vile kunywa pombe na mfano wake.

·       Kama mashirika ya kiserikali yatahusika katika kutakatisha basi haifai kuzitumia isipokuwa kwa idhini ya Faqihi mwenye masharti ya kufuatwa, kama ambavyo jambo ya kutakatisha si lenye kufaa kisheria.

Naam, inawezekana kukawa na vipengele vyenye kutoka katika hukumu hii, kama ambaye atakuwa anahitajia kutoa mali kwa ajili ya kufanya upasuaji wa dharura katika nchi nyingine, na nchi yake ikawa hairuhusu kutuma kiwango  kama hicho cha pesa, kiasi kwamba anatakiwa kuhamisha katika akaunti mbalimbali za watu, na jambo hili kwa asili kabisa haliingii katika anuani ya kutakatisha mali, na hata dharura pia inaipa anuani nyingine ya kwamba mali hizi ni halali.

Quran inasema “...Na mwenye kupata dharura bila yakuwa ni mwenye kutenda uovu wala uadui, basi Mwenyezi Mungu ni msamehevu na mwenye huruma...”[1].  Na hata katika hukumu mashuhuri ni kwamba kunapokuwa na dharura yenye kukatazwa huwa halali.

Hizi ndio hali ambazo zinajulikana katika jambo la kutakatisha mali, na natumia fursa hii kwa kuuhadharisha umma kunako hali nyingine ambazo si katika utakatishaji mali kwa maana ya kiuchumi, japokuwa bado zitakuwa na maana ile ile, kama vile kuhamisha pesa kwa zaidi ya njia moja ili kuweza kufikia lengo baya.

Na katika hayo ni mfano wa hila ambazo hutumika na baadhi ya watu kwa ajili ya kuweza kupata misimamo ya Marajii ili kuweza kutimiza malengo yao. Ambapo wanatumia baadhi ya watu kwa nembo ya kupeleka mali kwa marjii kwa jina la haki za kisheria, ambapo huaminiwa na kuweza kupatiwa lile ambalo analisema kwa marjii yule.

Au ikawa mtu ana lengo la kutenganisha jamii, ikawa yeye kama yeye hawezi kufanya hivyo, hivyo anaamua kumtumia mtu ambaye hana uelewa kwa kumpatia mali za kusimamisha vikao ambavyo ndani yake kutakuwa na maudhui za kutenga watu na jamii, ambapo kwa kufanya hivi yule mwenye lengo anafanikiwa.

Na mfano wa kihistoria wa jambo hili ni pale ambapo Ubeidu Llah Bin Ziyad alitaka kujua sehemu ambayo Muslim bin Aqil alifikia mjini Kufa, ambapo alimpatia mshauri wake mali nyingi sana kwa lengo la kwenda kukaa na masahaba wa Muslim kiasi atawalaghai na kuweza uvujisha siri ya alipo Muslim, na ilijulikana fika kuwa harakati ya Muslim ilihitajia mali, na yeye akatumia vizuri fursa hii kwa kujifanya ni katika wapenzi wa Ahlu Bait mpaka pale Muslim bin Ausaja akampeleka alipo na yakatokea yaliyotokea.

Pia hapa ni vyema kuashiria utakatishaji wa aina nyingine, mfano ambao unafanywa na baadhi yao kwa kutakatisha baadhi ya magaidi ambao wameshiriki katika kuangamiza watu wa Iraq, Syria na kisha wakawa na lengo la kurejea kwao (Saudia) kwa lengo la kupata msamaha wa mfalme wao, hivyo huwarudisha kwa njia ya Indonesia na kisha kuingia Saudia baada ya kuwapa anuani ya kwamba walikuwa ni walinganiaji ambao walitoka kutimiza majukumu yao nje ya nchi. Na kwa mujibu wa ripoti ambazo nimezipata kutoka kwa baadhi ya viongozi wa Indonesia ni kwamba mamia mpaa sasa wamepita kwa njia hii.

Na haya yote nimeyataja ili jamii ziweze kutambua baadhi ya vitimbi vinavyolenga kuzigawa na kupenyeza chuki baina yao, ili uwanja uweze kuwa safi na mafisadi waweze kutimiza malengo yao.

 

 

                   Ayaotollah Mohammad Yaaqubiy

                       13 Safar 1436

                          6/12/2014



[1] Surat baqara aya 173

Shiriki swali

Hukumu ya kumwangalia mwanamke unayetaka kumuoa

Swali:

    Je, inafaa mwanaume kumwangalia mwanamke ambaye anataka kumuoa bila ya hijabu na kabla ya ndoa?, na ni viungo gani vingine ambavyo mwanaume anaweza kuviangalia kwa huyo mwanamke kabla yandoa?.

 

Jawabu:

       Kwa jina la Mwenyezi Mungu

Inatosha kwake kumwangalia uso na viganja vyake tu, na kama atakuwa anataka kumwangalia zaidi basi atumie wanawake wa upande wake kumwangalia vizuri au kwa kuhofia kwamba inawezekana akawa na aibu.

                                                        Ayaotollah Mohammad Yaaqubiy

Shiriki swali

Hukumu ya uchafuzi wa mazingira.

Swali:

    Ni ipi hukumu ya uchafuzi wa mazingira, hasa uchafuzi ambao unapeleka madhara makubwa katika jamii kama vile swala la kupanda kwa joto, au kuchafua kabisa anga ambayo yatapelekea kuangamia watu wengi katika miji?.

 

Jawabu:

       Kwa jina la Mwenyezi Mungu

Ni haramu na haifai kabisa kufanya jambo lolote ambalo litapelekea mubashara madhara au maslahi ya watu.

                                                        Ayaotollah Mohammad Yaaqubiy

Shiriki swali

Tafsiri ya aya ya 6 katika Surat jathiya.

Swali:

Katika Suratu Aljathiya aya ya 6 tunasoma “.......Hizi Aya za Mwenyezi Mungu tunakusomea kwa haki; basi hadithi gani watakayo iamini baada ya Mwenyezi Mungu na Aya zake?...”. Sasa nina rafiki yangu ambaye anadai kuwa aya hii ni dalili tosha katika kuonyesha kutokuwa na haja ya Hadithi, sasa ni vipi naweza mueleza maana ya aya hii?.

Jawabu:

       Kwa jina la Mwenyezi Mungu

Umuhimu wa hadithi umethibitishwa na Quran yenyewe, “.....Yale anayokupeni Mtume yachukueni, na anayokukatazeni basi yaacheni.....”. Pia anasema “.....Na nakuapia kuwa hawatokuamini mpaka pale utakapowahukumu kunako wenye kutofautiana.....”. pia anasema “.....Na wala hakuwa ni mwenye kutamka kwa matamanio, isipokuwa ni ujumbe alioshushiwa tu....”. Pia anasema “....Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu, Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,  Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!...”.

Pia kama kusingekuwa na haja au umuhimu wa hadithi basi kwanini Mwenyezi Mungu kamtuma Mtume wake, na kisha kuendelea kumpa Wahyi hasa kwa kuzingatia angeweza kuishia katika Quran....?”.                                                       Ayaotollah Mohammad Yaaqubiy

Shiriki swali

Muamala wa mke kwa mume mwenye kudhihirisha maasi.

Swali:

Mimi kama mwanamke wa Kiislamu nikiwa na familia yenye watoto, vipi nitaweza kuamiliana na mume ambaye huwezi kumsifu kuwa ni Mwislamu kwa maana yake?, kwani haswali wala hafungi na ni mwenye kudhihirisha maasi waziwazi.

 

Jawabu:

       Kwa jina la Mwenyezi Mungu

Ikiwa huyo mume hatakuwa ni mwenye kuacha kuwatimizia majukumu yake ya lazima kama vile chakula na malazi, na hakuwa ni mwenye kuwalazimisha kuacha mambo ya lazima kama vile swala na funga ya Ramadhani, au kufanya vitendo vya haramu kama vile kuvua hijabu mbele ya watu basi vumilia kwanza. Mpe nasaha kwa maneno yahekima na mazuri, na usimwambie maneno ambayo yatampelekea kuwa sugu na kupinga zaidi.

Kama ambavyo ni muhimu mno pia kukaa na watoto wako na kuzungumza nao juu ya malezi sahihi na wakawa na imani na wewe zaidi. Inshallah Mwenyezi Mungu atakusaidia katika jukumu hili.

                                                        Ayaotollah Mohammad Yaaqubiy

Shiriki swali

Hukumu ya kuchunguza maiti (baada ya kifo)

Swali:

 Ni upi tazamo wenu kunako jambo hili?

     Kuchunguza maiti kutokana na amri za mahakama au vitengo vyenye kuhusika na uhakiki wa vifo, jambo ambalo husimamiwa na madaktari waliobobea katika kuchunguza mwili wa mwanadamu ili kujua sababu asili ya kifo?.

Jawabu:

Kwanza haifai kukata kiungo cha maiti kutokana na uharamu wa jambo hili, kama ambavyo ni haramu akiwa hai pia. Naam, kama kufanya hivyo itakuwa kuna maslahi kama vile kuthibitisha kutohusika mtuhumiwa, kupatikana kwa haki ya mtu mwingine, au kuweza kuamua baina ya pande mbili, au kuondoa madhara yenye kusimamia jambo hilo basi kutakuwa hakuna shida.

Lakini kuweza tu kujua sababu ya kifo haitoshi kuwa sababu ya kufanya hayo, na tumejitahidi sana kuwaelewesha wataalamu kunako umuhimu wa kushikamana na hukumu za kisheria na kubakia katika zile sehemu ambazo wameruhusiwa tu. Na kama hawatafanya hivyo basi watakuwa wametenda makosa makubwa mno (Mungu atuepushe mbali), kama ambavyo mwenye kutenda jambo hilo atatakiwa kutoa dia kwa wenye maiti, na kiwango cha dia hiyo kimetajwa katika risala.

                                                        Ayatollah Mohammad Yaaqubiy

                                                                28 Muharram 1436

                                                                         21/11/2014

Shiriki swali

Hukumu ya kumvutia taswira mwanamke ambaye si halali kwako.

Swali:

    Ni ii hukumu ya mtu kumvutia picha na taswira mwanamke ajnabi (ambaye si halali kwake)?.

 

Jawabu:

       Kwa jina la Mwenyezi Mungu

Kwanza kabisa swala la fikra si katika uwezo wa binadamu, lakini cha muhimu ni kwamba fikra na hizo taswira zisipelekee kuangukia katika mambo ya haramu. Hali kadhalika ni wajibu kuweza kujitahidi kwa kadri yako kuweza kuacha kufikiria, na jitihada i jambo lenye kuwezekana.

                                                        Ayaotollah Mohammad Yaaqubiy

 

Shiriki swali

Kufanya kazi na wenye kutozingatia dini.

Swali:

    Kutokana na uhaba wa ajira, nimejikuta katika sehemu ambayo nafanya kazi ya mgahawa, lakini mmiliki wake ni mtu ambaye hana tabia nzuri, nami nimejitahidi sana kumpa nasaha lakini mwisho wa siku anarejea katika kawaida yake. Je, kufanya kazi na mtu kama huyu inafaa?.

 

Jawabu:

       Kwa jina la Mwenyezi Mungu

Hakuna kizuizi katika kufanya naye kazi, na usiache kumpa nasaha na mawaidha ili aweze kuzinduka na kukumbuka. Dua zangu zipo pamoja nawe.

                                                        Ayaotollah Mohammad Yaaqubiy

1 2 3 4 5
total: 41 | displaying: 11 - 20

Ofisi ya al-Marjii Wadini

Khekhe Muhammad Yaqoobi (Allah amhifadhi) - Tuma swali lako-

Najaf Ashraf