Ayatollah Yaaqobiy akemea kila lenye kusababisha tofauti na mifarakano.

| |times read : 1131
  • Post on Facebook
  • Share on WhatsApp
  • Share on Telegram
  • Twitter
  • Tumblr
  • Share on Pinterest
  • Share on Instagram
  • pdf
  • Print version
  • save

Ayatollah Yaaqobiy akemea kila lenye kusababisha tofauti na mifarakano.

Swali:

             Assalamu Alaykum

Kumekuwa na kudhihiri baadhi ya wakati mambo ya kusema vibaya viashiria vya itikadi fulani za kidini kwa namna moja au nyingine, ni upi msimamo wenu katika kuelekea jambo kama hili?.

 

Jawabu:

Kwa jina la Mwenyezi Mungu

Amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yako pia.

Msimamo wetu katika jambo hili upo wazi mno, kwani katika maelezo yetu mbalimbali tumekataza jambo hili, kutokana na kuwa ni kinyume na mienendo ya maimamu wetu watukufu na maelekezo yao kwa wafuasi wake.

Bila shaka jambo hili husababisha mizozo na mifarakano, hali yakuwa Mwenyezi Mungu ameshasema kuwa “.....Wala msigombane kwani itapelekea kushindwa kwenu....” Surat Anfal aya 46.

Na kila ambapo kutakuwa kuna mambo mengi ambayo makundi mawili wanashirikiana (Suni na Shia), basi jambo hili lichungwe maradufu, na kama tutashindwa kuunganishwa na haya tunayoshirikiana basi tuungane kwa kumuangalia adui yetu ambaye hachagui wa kumuangamiza katika sisi, na wala kwake si aibu kuangamiza chochote kile hata kama kitakuwa kitukufu katika matukufu yetu.

Inshallah Mwenyezi Mungu ndio msaidizi wa yote.

Ayatollah Yaaqubiy

15/2/1436

5/4/2015