Mwezi wa Rajabu ni kituo cha neema za Mwenyezi Mugu:

| |times read : 509
  • Post on Facebook
  • Share on WhatsApp
  • Share on Telegram
  • Twitter
  • Tumblr
  • Share on Pinterest
  • Share on Instagram
  • pdf
  • Print version
  • save

Mwezi wa Rajabu ni kituo cha  neema za Mwenyezi Mugu:

Hakika  mwezi wa Rajabu unaandaa mazingira, na sehemu muwafaka kwa ajili ya kuyapata maarifa ya kumtambua Mwenyezi Mungu aliyetakasika, kwa sababu ni moja ya vituo vya neema maalumu za Mwenyezi Mungu,vile vile ni katika sababu alizoziweka Mwenyezi Mugu, ili kuipata Ridhiwani yake (ridhaa yake). Hivyo, yeyote atakayeyatafuta hayo kwa Mwenyezi Mungu na akayafanyia juhudi, bila shaka Mwenyezi Mungu atampa, kwani hii ni ahadi yake aliyoitoa kwa mtume wake (s.a.w.w). hakika imepokelewa kutoka kwa Mtume (s.a.w.w) kwamba, alisema: “Hakika Mwenyezi Mungu alimuweka malaika anayeitwa Dai’I (muitaji) katika mbigu ya saba, basi uingiapo mwezi wa Rajabu yule malaika hunadi kila uingiapo usiku mpaka asubuhi, akisema: “Raha wanayo wenye kufanya dhikiri, raha wanayo wenye kutii, na Mwenyezi Mungu aliyetukuka anasema: Mimi ni mwenye kukaa na mwenye kukaa nae, na ni mwenye kumtii anayenitii, na ni mwenye kusamehe mwenye kuniomba msamaha, Mwezi ni wangu, na mja ni wangu, na huruma ni yangu, basi atakayeniomba ndani ya mwezi huu nitamjibu dua yake, na atakayeniomba nitampa, na atakayetaka hidaya kwangu nitamuongoza, na nimeufanya mwezi huu kuwa ni kwamba baina yangu na waja wangu, atakayeambatana nayo bila shaka atafika kwangu”.