Kuhuisha (kudumisha) Majalisi (vikao) za Ahlul-bayt (a.s):

| |times read : 488
  • Post on Facebook
  • Share on WhatsApp
  • Share on Telegram
  • Twitter
  • Tumblr
  • Share on Pinterest
  • Share on Instagram
  • pdf
  • Print version
  • save

Kuhuisha (kudumisha) Majalisi (vikao) za Ahlul-bayt (a.s):

 

Hakika kudumisha kumbukumbu za Ahlul-bayt (a.s) na kuzitaja sifa zao, sio historia isimuliwayo wala vitu vya kale viwekwavyo kwenye majumba ya makumbusho, bali kufanya hivyo ni chanzo na chemchemi inayokusudiwa na kila kiongozi, msuluhishi, mwanafikra, msomi, mlezi na kila msaka haki na heri. Nalo ni mwanga unaomuangazia wanadamu njia ya imani ya kweli, maadili mema na maisha ya furaha. Ahlul-bayt (a.s) hawakutuachia jambo dogo wala kubwa, isipokuwa waliliwekea kanuni sahihi, hata katika yale mambo ya kawaida maishani ambayo ni mara chache watu huyapa umuhimu, kama vile: kula, kufanya tendo la ndoa, kwenda msalani, kulala, kuingia bafuni na mfano wa hayo, ambayo sheria na kanuni za kibinadamu huyakosa na hivyo kushindwa kuikidhi mahitaji yote ya mwanadamu.