Hebu tujiulize...
10/07/2020 09:33:00 |
18/Dhul-Qadah/1441|times read : 490
Hebu tujiulize...
“...Hebu kwa pamoja tujiulize swali hili, Ni kipi mwanadamu atapoteza endapo atamtii Mwenyezi Mungu katika sheria zake?. Kwa hakika hatopoteza kitu, bali kinyume chake kabisa ni kwamba ataishi maisha ambayo anayaishi mwenye kumuasi Mungu (Raha), tena hata zaidi ya hapo, kwa maana huyu atakuwa na raha za dunia na ahera kwa pamoja ambazo zinasababishwa na hii imani yake kwa Mwenyezi Mungu swt. Mwenyezi Mungu anasema “..Na hakika nyinyi mnataraji kutoka kwa Mwenyezi Mungu mambo ambayo wao (makafiri) hawataraji..”.