Funga siku ya shaka
09/07/2020 21:26:00 |
18/Dhul-Qadah/1441|times read : 417
Funga siku ya shaka
Swali:
Ni ipi hukumu ya kufunga siku ya shaka, siku ambayo hatujui kuwa inakamilisha mwezi wa Shaabani au ni tarehe mosi Ramadhani, hasa ikiwa hatuna uhakika wa kuandama kwa mwezi.
Jawabu:
Kufunga siku kama hii kwa anuani ya kuwa ni Ramadhani si sahihi na batili, na hata kutokujua unanuia nini pia ni batili, kwani lazima ujue kuwa unafunga Shaabani ambayo ni Suna, au Ramadhani ambayo kwa hapa si sahihi. Ila unaweza kuifunga kwa anuani ya kulipiza yaliyo katika dhima yako, na hii itajitosheleza itakapokuja bainika kwamba ni kweli ilikuwa Ramadhani.
Ayatollah Sheikh Muhammad Yaaqobiy