Hukumu za mazungumzo ya kimitandao baina ya jinsi mbili tofauti

| |times read : 347
  • Post on Facebook
  • Share on WhatsApp
  • Share on Telegram
  • Twitter
  • Tumblr
  • Share on Pinterest
  • Share on Instagram
  • pdf
  • Print version
  • save

Hukumu za mazungumzo ya kimitandao baina ya jinsi mbili tofauti

Swali:

 Ni ipi hukumu ya mwenye kuzungumza na binti kwa njia za simu au mitandao ya kisasa kwa lengo la kumuongoza au kujadiliana naye maswala ya kijamii yenye manufaa, hasa pale ambapo mtu huyu akawa anamchukulia binti huyu kama dada yake ambaye anaweza kusikia sauti yake na kuzungumza naye muda wowote, kama ambavyo akatoa hoja kwamba baina yao haiwezekani kukazalikana matamanio?.

 Tunaomba mwongozo wako Shekhe wetu.

Jawabu:

Kwa jina la Mwenyezi Mungu.

   Siku zote mahusiano  kama haya hayawi na natija nzuri, maana mara nyingi mno hupelekea kuangukia katika kutenda dhambi, na hii ni kutokana na mahusiano ya kinyoyo ambayo hupatikana, kama ambavyo tajiriba inaonyesha hivyo.

Pia haiwezekani kuainisha lengo ( kama hivyo kumuongoa kama idhaniwavyo), kwa maana hilo lengo linaweza kupatikana kupitia jinsia yake mfano kupitia  chuo cha Zahraa na vinginevyo kwa njia ambayo itawezekana kuwaweka wanawake sehemu moja.

Na ni muhimu sana kukaa mbali na vitimbi vya shetani ambaye huanzia na nukta sahihi kisha baadaye hukengeuka. “....na wala msiwe ni wenye kufuata vitimbi ya shetani...”[1]                             

                                                            Ayatollah Mohammad Yaaqubiy



[1] Surat Baqara aya 168