Hukumu ya kubakia katika kuwafuata Marajii waliopita, pamoja na kufanyia kazi Ihtiyat za wajibu

| |times read : 367
  • Post on Facebook
  • Share on WhatsApp
  • Share on Telegram
  • Twitter
  • Tumblr
  • Share on Pinterest
  • Share on Instagram
  • pdf
  • Print version
  • save

Hukumu ya kubakia katika kuwafuata Marajii waliopita, pamoja na kufanyia kazi Ihtiyat za wajibu

Swali:

    Kwako Ayatollah Sheikh Mohammad Yaaqubiy, amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yako.

Tunaomba fatwa yako katika hili na Mwenyezi Mungu atwalipa, Je, mnaruhusu mtu kubakia katika kumfuata Ustadh Sayyid Al Khui (ra) na maulama wengine waliopita?.

Na je inawezekana mtu kumrejea mwingine asiyekuwa wewe katika mambo ya ihtiyat za wajibu?.

                                    Kikundi cha wenye kumfuata Sayyid Al Khui (ra). 

 

Jawabu:

       Kwa jina la Mwenyezi Mungu

Sisi tunaruhusu kwa waliokuwa wakimfuata Sayyid Khui na Shahid Sadr (wote wawili) kubakia katika kutendea kazi risala zao, lakini katika maswala ambayo yanatokea zama hizi pamoja na yale ambayo yanajulikana kabisa tofauti zake basi ni lazima warejee kwangu. Na idhini hii itabakia mpaka pale tutakapotoa tamko lingine kwa uwezo wa Mungu.

Pia sisi tunamlazimisha mtu kufanyia kazi Ihtiyat za wajibu zilizotajwa katika vitabu. lakini itakapokuwa kuna tatizo na ikawa mtu anataka ufafanuzi zaidi basi aturejee, maana huenda lile ambalo tunaruhusu arejee kwa wengine ikawa ni katika mambo ambayo yanatakiwa kufuata mwenye elimu zaidi, kwani si kila mambo ya ihtiyat za wajibu inawezekana kurejea kwa mwingine.

                                                        Ayatollah Mohammad Yaaqubiy