Hukumu ya kutukana baadhi ya alama za madhehebu za Kisuni.
Hukumu ya kutukana baadhi ya alama za madhehebu za Kisuni.
Swali:
Ilikuwa ni katika siku ya kukumbuka kifo cha Imamu Muhammad Jawad (as), ambapo kundi la vijana lilitoka huku wakiwa wanatukana baadhi ya alama za ndugu zetu Masuni, ni upi msimamo wenu katika jambo hili?.
Jawabu:
Kwanza huu ni ujinga na uumbavu ambao kwa namna yeyote ile hauwezi kunasibishwa na mafunzo ya Ahlu Bayt (as), na naona kabisa kuna umuhimu wa kuwepo vikundi maalumu vyenye kuelekeza watu kama hawa uwepo wa fitina hizi. Na tumeshaashiria hapo mwanzo tulipokuwa tunazungumzia (Mbinu za kishetani tulizoandaliwa) na tukawaonya watu kunako hilo.
Ayatollah Mohammad Yaaqubiy
7 Dhul Hijja 1434