Hukumu ya gemu la Clash of Clans

| |times read : 418
  • Post on Facebook
  • Share on WhatsApp
  • Share on Telegram
  • Twitter
  • Tumblr
  • Share on Pinterest
  • Share on Instagram
  • pdf
  • Print version
  • save

Hukumu ya gemu la Clash of Clans

Swali:

Katika masiku ya karibuni kumeenea sana mchezo wa simu za kisasa na kompyuta mpakato kwa jina la (Clash Of Clan), na umetokea kpoteza mno muda wa vijana na hata kupelekea baadhi yao kuuziana kwa bei za juu mno. Mchezo huu umesimamia katika kuunda majeshi na miji na kisha kushambuliana kwa ajili ya kupata pointi, na kila ambapo pointi za mji fulani zinapanda basi ndivyo ambavyo bei yake huwa juu. Na kama mnavyotambua ni kwamba michezo mingi ya sasa huwa imetengenezwa kwa lengo la kupandikiza uadui katika nyoyo za watoto na vijana, ukiongezea kutekwa na michezo hii kwa muda mrefu mno, iwe majumbani au hata maukumbi ya michezo kiasi kwamba maadili na tabia za vijana na watoto yanaathirika kwa kiwango kikubwa mno.

Je, mna ruhusu watu kucheza na kuingia katika kumbi na hii michezo?.

Tunaomba mwomgozo na Mwenyezi Mungu atawalipa.

 

Jawabu:

Baada ya kuchunguza na kufuatilia tumekuta kwamba katika mchezo huu kuna mambo mengi ambayo yanapelekea kushiriki uchezaji wake, na tuna mengi sana ambayo tumeyaongea tangu mwaka 2003 katika kuelezea hatari za michezo hii katika akili za watu, jamii, tabia, dini na hata kiuchumi, na hili peke yake linatosha kuwa kigezo cha kuzuia.

Hivyo tunawashauri wakuu na wasimamizi kuweza kuwadhibiti watoto wao na mienendo yao, kama ambavyo tunaomba wenye mamlaka husika waweze kuchukua hatua zuizi kwa hizi sehemu na kumbi za hii michezo, bila ya kuangalia kwamba zinaingiza pesa. Na hii ni kwa ajili ya kuokoa kizazi cha watoto wetu, na Mwenyezi Mungu atatusaidia.

Ayatollah Muhammad Yaaqubiy

8 Rabiul Thani 1437H