Marjii Ayatollah Yaaqubi, ahimiza ofisi zake za kielimu na kijamii kusaidia vitabu katika Chuo Kikuu cha Mousil pamoja na kuimarisha upya majengo yake.

Marjii Ayatollah Yaaqubi, ahimiza ofisi zake za kielimu na kijamii kusaidia vitabu katika Chuo Kikuu cha Mousil pamoja na kuimarisha upya majengo yake.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mtukufu
Marjii Ayatollah Yaaqubi, ahimiza ofisi zake za kielimu na kijamii kusaidia vitabu katika Chuo Kikuu cha Mousil pamoja na kuimarisha upya majengo yake.
Na pia Ayatollah Yaaqubiy ameashiria kwamba uharibifu wa kifikra na kijamii ambao umefanywa na vikundi vya kigaidi katika miji waliyoingia na kuvamia, ni wa hatari zaidi kuliko hata ule wa kimada unaofanywa na majeshi au maaskari wavamizi, na kwamba jambo la kumkomboa mwanadamu ni gumu zaidi ya kukomboa ardhi. Kwani inahitajia muda mrefu ili kuweza kusafisha tena nidhamu ya kifikra na kitabia au hata itikadi hasa kwa watoto na vijana. Saa kueneza na kuandaa vitabu vyenye maudhui ya kutuliza na kujenga misingi ya kibinadamu ni katika baadhi ya njia ambao zinaweza kumkomboa mwanadamu.
Aidha pia Kiongozi huyo amehimiza taasisi zote za kielimu kushiriki ipasavyo katika jambo hili, huku akizitaka serikali zote husika kushirikiana nao katika jambo hili na kulipa kipaumbele zaidi. Na Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kuelekewa.
Kitengo cha habari Ofisi ya Ayatollah
Sheikh Muhammad Yaaqubiy
25 Rabiul Thani 1438
24/1/2017