Hukumu ya Mafuta yanayotumika kulainisha uso
04/07/2020 19:29:00 |
12/Dhul-Qadah/1441|times read : 479
Hukumu ya Mafuta yanayotumika kulainisha uso
Swali:
Kutokana na hali ya baridi watu huwa wanatumia mafuta kwa ajili ya kulainisha ngozi zao, na hali hii huwa ni kwa wingi na endelevu, sasa vipi mtu akawa anataka kuchukua udhu huku akiwa anajua kabisa kwamba masaa machache kabla alitumia mafuta?, je achukue udhu hivyohivyo au ni lazima kwanza aondoe mafuta yote?.
Jawabu:
Kwa Jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma na mwenye kurehemu.
Ikiwa ambayo yamebakia ni mafuta ambayo hayazuii kufika kwa maji katika viungo vya udhu basi hakuna tatizo, lakini kama itakuwa yaliyobakia ni ukungu mzito basi ni lazima autoe kwanza.
Ayatollah Sheikh Muhammad Yaaqobiy